Star Tv

Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Babati mkoani Manyara Yonna Keawo ametoa muda  wa miezi minne,  kuhakikisha  fedha zote zilitotengwa na halmashauri hiyo  kwa ajili ya kukamilisha  baadhi ya miradi ya maendeleo iliyoanzishwa  kwa nguvu za wananchi,  zinapelekwa kwenye miradi hiyo.

Taarifa na  Zacharia Mtigandi

Add a comment

Wizara ya Maliasili na Utalii imetangaza kuanza kutoa vibali rasmi vya kuanzisha mashamba na bucha za Wanyamapori  kwa watanzania wenye kipato cha chini ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo liilotolewa na rais wa Jamhuri ya Muungano Dokta John Magufuli Oktoba 10 mwaka 2019 alipokuwa ziarani Mkoani Katavi.

Taarifa na Beatrice Gerald.

Add a comment

Wananchi  wanaoishi maeneo ya pembezoni  mkoani Arusha  wameiomba serikali kuwapelekea madaktari bingwa katika vituo vya afya vinavyojengwa katika maeneo yao ili kuwapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu nakutumia gharama kubwa.

Taarifa na Beatrice Gelard.

Add a comment

Tanzania imeutaka Umoja wa Afrika na Jumuiya za Kimataifa kuongeza jitihada za kuleta amani katika maeneo yenye migogoro Barani afrika hususani katika Nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ili kuipunguzia Tanzania idadi kubwa ya wakimbizi

Add a comment

Gavana wa Benki kuu Tanzania Florens Luoga amesema muda sio mrefu itaweka kanuni za kuhakikisha fedha zinazotokana na madini zinarudi Nchini kwani wawekezaji walikua wnadanganya kwa sababu ya kuwa na akaunti za benki nje ya nchi na kusababisha fedha kutorudi Nchini.

Taarifa na Salma Mrisho.

Akiwa Mkoani Geita kwa ziara ya siku moja na kutembelea mgodi wa dhahabu wa geita pamoja na maeneo mengine kuangalia hali ya uzalishaji wa dhahabu unavyofanyika.

Luoga  amesema kuwa haiwezekani Tanzania kuwa na dhahabu za kutosha halafu hakuna eneo la kuhifadhi dhahabu na kuongeza kuwa hivi karibuni kutakua na kanuni za uhifadhi wa dhahabu.

Uwepo wa masoko ya dhahabu umechangia kupatikana kwa mapato ambapo kuanzia machi 2019 hadi januari 2020 umeshazalisha tani tatu za Dhahabu zenye thamani ya bilioni 362.

Suala la kituo cha kuhifadhi dhahabu nalo limezungumzwa na kuonekana kama changamoto inayowakabili wawekezaji hao ambapo BOT wamesema  watakaa na kulifanyia kazi.

Halmashauri ya Mji wa Geita tayari imetenga maeneo ya kimkakati kwa shughuli mbalimbali za sekta ya madini.

                                                           Mwisho.

 

 

Add a comment

Mamlaka ya kuthibiti na kupambana na dawa za kulevya nchini imemkamata mwekezaji raia wa Poland Damian Sanikowsiki (40) kwa tuhuma za kuzalisha na kumiliki shamba la bangi, Kata ya Njia Panda Mashariki eneo la Mji mdogo wa Himo Wilaya ya Moshi.

 Taarifa na Rodrick Mushi

Kaimu Kamishna Jeneral wa mamlaka ya kuthibiti na kupambana na dawa za kulevya nchini james Kaji amesema wamefanikiwa kumkamata mwekezaji huyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema juu ya kilimo cha mazao ya bangi kilichokuwa kikiendelea kwenye eneo hilo ambalo limezungushiwa ukuta.

Kaimu Kamishna amesema kuwa mara baada ya kikosi kazi kufika katika eneo hilo mwekezaji alishawishi kutoa rushwa ya Tsh milioni 10 huku akiwaahidi kuendelea kuwapatia kiasi cha Tsh milioni 40 kila mwezi kwa ajili ya kumaliza suala hilo.

Kwa upande wake mwekezaji aliyekamatwa amesema amekuwa akifanya uzalishaji wa bangi na kwa ajili ya wateja wake wakubwa waliopo ndani na nje nchi..

Uongozi wa mtaa umesema mwekezaji huyo alinunua eneo hilo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto yatima na uwekezaji wa hoteli eneo ambalo ameligeuza kwa ajili ya kilimo haramu cha bangi.

                                                                           Mwisho

 

 

 

Add a comment

Basi la kampuni ya Premier linalofanya safari zake kati ya Mwanza na Mbeya limegongana uso kwa na lori lenye namba za usajili T486 ANU ambalo lilikuwa likivuta tela lenye namba T 775 APT na kusababisha vifo vya Watu wawili na majeruhi nane.

Ajali hiyo ambayo imehusisha basi na lori imetokea majira ya asubuhi  katika kijiji cha Inyala wilaya ya Mbeya mkoani Mbeya.

Jitihada zilofanywa ni kuliondoa lori ambalo lilikuwa limeegeshwa barabarani ili kuruhusu magari mengine yaweze kupita na kuendelea na safari kwenye barabara hiyo pamoja na  kuwakimbiza majeruhi hospitali.

                                                                 Mwisho.

 

Add a comment

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato na  kurahisisha ulipaji wa kodi zimewezesha mapato ya kodi kwa Disemba, 2019 kuvunja rekodi na kufikia sh. trilioni 1.92.

Waziri Mkuu amesema kuimarika kwa huduma za usafirishaji na mawasiliano, upatikanaji wa huduma ya maji, kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya kilimo, kuongezeka kwa uzalishaji wa madini hususani makaa yam awe na dhahabu kumekuwa chachu ya mafanikio ya kuongezeka kwa mapato hayo.

Amesema kwa upande wa matumizi ya fedha kuanzia mwezi July-Disemba 2019 serikali imetumia shilingi trilioni 15.32 ambazo ni sawa 91.25% ya lengo ambapo fedha hizo zimetumika kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo na uendeshaji wa shughuli za serikali katika wizara pamoja na ugharamiaji wa deni la serikali pamoja na kazi nyinginezo.

Aidha, waziri mkuu amesema kuongezeka kwa mapato hayo kumeiwezesha serikali kuendelea kuwahudumia wananchi kupitia ujenzi na uboreshaji wa miundombinu mbalimbali kwa ajili ya shughuli za ujenzi wa uchumi na kijamii.

Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililotamatishwa na mkutano wa 18 limeahirishwa leo kwa hotuba ya waziri mkuu ambayo ndani yake imetaja kuongezeka kwa mapato ya taifa.

                                                              Mwisho.   

Add a comment

Takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania ni kitovu cha uhifadhi wa simba duniani kutokana na kuwa na wanyamapori hao wanaokadiriwa kufikia zaidi ya elfu kumi na saba ambao wamekuwa kivutio kikumbwa kwa wageni wanaoingia nchini kujionea rasilimali hiyo muhimu katika hifadhi za taifa.

Taarifa na Sadick Hunga…….

Add a comment

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.