Star Tv

Wizara ya Maliasili na Utalii imetangaza kuanza kutoa vibali rasmi vya kuanzisha mashamba na bucha za Wanyamapori  kwa watanzania wenye kipato cha chini ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo liilotolewa na rais wa Jamhuri ya Muungano Dokta John Magufuli Oktoba 10 mwaka 2019 alipokuwa ziarani Mkoani Katavi.

Taarifa na Beatrice Gerald.

Akizungumza na Wanahabari Mkoani Arusha ,Waziri wa Wizara hiyo Dokta Hamis Kigwangala amesema Wizara hiyo tayari imeanza hatua za awali ikiwemo marekebisho ya sheria pamoja na kushusha ada ya uanzishaji mashamba hayo.

Dokta Kingwangala amesema biashara hiyo itafanyika kwa msimu mzima wa mwaka kwa wafanyabiashara wenye mashamba ya wanyamapori ambao watakuwa wamekidhi vigezo.

Ujio huo wa maduka ya nyamapori inapokelewa kwa hisia tofauti na baadhi ya wakazi mkoani Arusha ambao wamesema kuwa fursa hiyo itakuwa chanzo kingine cha mapato kwa Wizara hiyo ambayo imekuwa ikitegemea shughuli za Utalii.

Uanzishwaji wa maduka hayo ya nyamapori unatajwa kuja kupunguza Uhalifu hasa Ujangili,huku Walengwa wakuu wa ulaji wa Nyama hiyo wakitajwa kuwa ni Watanzania wanaoishi kwa kipato cha Chini.

                                                                                               Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.