Star Tv

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ametangaza maombolezo ya kitaifa baada ya kufariki Rais wa pili wa nchi hiyo, Daniel Arap Moi.

Mzee Moi ambaye amefariki asubuhi ya leo hospitali ya Nairobi  akiwa amezungukwa na familia yake mpaka sasa ratiba ya mazishi bado haijawekwa hadharani.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu ya Kenya imesema muda wa maombolezo utaisha baada ya mazishi ya Mzee Moi.

Katika kipindi chote cha maombolezo, bendera ya Kenya itapeperushwa nusu mlingoti kwenye majengo na ofisi zote za umma, jeshi na ofisi za ubalozi wa nchi hiyo kote duniani.

Baadhi ya wananchi wa Kenya wametoa salamu zao juu ya kifo cha Rais Moi ambapo miongoni mwao wamesema kwa muda wa miaka 24 ya utawala wa Mzee Moi kutoka 1978 mpaka 2002 ilikuwa ni mchanganyiko wa maendeleo na utawala wa mkono wa chumai.

Taarifa zimeeleza kuwa jeshi la nchini Kenya litaongoza mipango yote ya mazishi ya Amiri Jeshi huyo mstaafu wa nchi hiyo.

Viongozi mbalimbali  wametuma salamu zao za rambirambi akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe  Magufuli ameandika katika ukarasa wake wa twitter

"Kwa niaba ya Serikali na Watanzania nakupa pole Mhe.Rais Uhuru Kenyatta na Wakenya wote kwa kuondokewa na Rais Mstaafu Daniel Toroitich arap Moi. Watanzania tutamkumbuka kwa uongozi wake mahiri, jitihada za kuimarisha uhusiano wetu na Kenya na kufufua Jumuiya ya Afrika Mashariki."

Viongozi wengine  waliotuma salamu za rambirambi  kwa familia ya Rais Moi na nchi ya Kenya ni pamoja na Waziri Mkuu wa Ethiopia pamoja na balozi wa Marekani nchini Kenya Kyle McCarter

                                                                                       Mwisho.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.