Star Tv

Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika limeitisha kikao cha dharura hii leo kujadiliana hali ya kisiasa na usalama nchini Sudan.

Jeshi la Sudan na kikosi maalumu cha wanamgambo cha Rapid Support Forces, RSF wameendelea kwa siku ya pili kupambania udhibiti wa taifa hilo, hali inayoashiria kutokuwa tayari kumaliza uhasama licha ya kuongezeka kwa shinikizo la kidiplomasia la kusitisha mapigano.

Mapigano makali ya ardhini na angani yameshuhudiwa hii leo katika mji mkuu, Khartoum na mji unaopakana nao wa Omdurman pamoja na maeneo mengine yanayozozaniwa nchini humo. Kulingana na Kamati Kuu ya madaktari nchini Sudan, watu 56 wameuawa ikiwa ni pamoja na watumishi watatu wa shirika la Mpango wa chakula ulimwenguni, WFP. Shirika hilo limetangaza kusitisha kwa muda shughuli zake nchini humo. Umoja wa Mataifa umelaani mauaji ya watumishi hao waliokuwa wakitekeleza majukumu yao.

Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika limeitisha kikao cha dharura hii leo kujadiliana hali ya kisiasa na usalama nchini Sudan, hii ikiwa ni kulingana na taarifa kupitia ukurasa wa Twitter. Katika hatua nyingine, Misri kupitia mwakilishi wake kwenye Muungano wa mataifa ya Kiarabu, imezitaka pande zinazohasimiana kuhakikisha usalama wa maslahi yake.

CHANZO: DW KISWAHILI

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.