Star Tv

Mama mmoja aitwaye Neema Joseph mkazi wa kijiji cha Burungu wilaya ya Musoma Mkoani Mara ameliwa na Mamba wakati akioga ndani ya Ziwa Victoria majira ya saa nne usiku katika ufukwe wa Bulungu.

Habari na Sadick Hunga ...

Add a comment

Serikali inakusudia kuzifuta ofisi za ardhi za kanda na kuanzisha ofisi za mikoa ambazo zitashughulikia masuala yote ya ardhi ili kuondoa urasimu na kusogeza huduma karibu na wananchi.

Habari na Laudence Simkonda.

Add a comment

Mamlaka ya wanyamapori wilayani Serengeti imelazimika kumuua kwa risasi mnyama aina ya chui baada juhudi za kumrejesha kwenye hifadhi kugonga mwamba ambapo inadaiwa chui huyo alivamia makazi ya watu katika Kijiji cha Bisarara mapema siku ya Jumanne na kusababisha madhara ikiwemo kuua mifugo na kujeruhi watu sita.

Add a comment

Mawakala inayotekeleza zoezi la usajili wa laini za simu kwa alama za vidole mkoani Njombe wameitupia lawama mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA kwa kuchelewa kukamilisha zoezi hilo kwa wakati. 

 Habari na Dickson Kanyika.

Add a comment

Kiongozi wa Harakati la Sadr nchini Iraq ametoa wito kwa wananchi  kufanya maandamano ya watu wasiopungua milioni moja ya kulaani kuwepo kijeshi Marekani nchini humo.

Add a comment

Aliyewahi kuwa  katibu  wa baba wa Taifa hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mzee Samuel Kasori amesikitishwa na hatua ya serikali ya kukitelekeza chuo cha utafiti wa kilimo na  mifugo Uyole jijini Mbeya, ambacho kilianzishwa na mwalimu Nyerere kwa misingi maalumu ya kukuza na kuendeleza sekta ya kilimo nchini.

Add a comment

Naibu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amewasimamisha kazi wahandisi wote wa Maji Wilaya ya Busega RUWASSA wanaosimamia mradi wa maji Lamadi na kuagiza wapangiwe kazi nyingine, huku akiwaweka ndani watu wanne, wakiwemo wahandisi wawili washauri wa mradi, kutokana na kushindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo katika usimamizi wa mradi wa maji Lamadi unaojengwa na serikali kwa gharama ya shilingi bilioni 12.8.

Add a comment

Naibu wa  Waziri wa Ardhi Nyumba na  maendeleo ya Makazi  Angelina Mabula amesema wakulima  wanapaswa kupimiwa maeneo yao ili kutokemeza migogoro ya ardhi nchini kwakuwa wataweza kujipatia hati miliki  ya ardhi zao.

Add a comment

Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour Party TLP Augustino Mrema ameitaka Serikali kumlipa Shilingi bilioni mbili kama fidia ya kesi alizowahi kushtakiwa chini ya serikali ya awamu ya tatu iliyokuwa inaongozwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa.

Add a comment

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.