Rais Dokta John Pombe Magufuli amewaapisha viongozi mbalimbali leo Februari 03,2020 ambao aliwateua hivi karibuni.
Akizungumza katika hafla ya kuwaapisha viongozi hao iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salam, Rais Magufuli amewataka viongozi hao kufanya kazi kwa bidii
Viongozi walioapishwa kwenye hafla hiyo ni pamoja na Makatibu wakuu watano na Naibu Katibu Mkuu mmoja, Makatibu Tawala wa Mikoa Mitatu, Kamishina Jenerali wa Magereza pamoja na Kamishina Jenerali wa Zimasmoto na Uokoaji.
Wengine ni pamoja na Kamishina wa Ardhi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Msajili wa Mahaka ya Rufani pamoja na Msajili wa Mahakama Kuu na Wajumbe watatu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama.
Mwisho