Star Tv

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato na  kurahisisha ulipaji wa kodi zimewezesha mapato ya kodi kwa Disemba, 2019 kuvunja rekodi na kufikia sh. trilioni 1.92.

Waziri Mkuu amesema kuimarika kwa huduma za usafirishaji na mawasiliano, upatikanaji wa huduma ya maji, kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya kilimo, kuongezeka kwa uzalishaji wa madini hususani makaa yam awe na dhahabu kumekuwa chachu ya mafanikio ya kuongezeka kwa mapato hayo.

Amesema kwa upande wa matumizi ya fedha kuanzia mwezi July-Disemba 2019 serikali imetumia shilingi trilioni 15.32 ambazo ni sawa 91.25% ya lengo ambapo fedha hizo zimetumika kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo na uendeshaji wa shughuli za serikali katika wizara pamoja na ugharamiaji wa deni la serikali pamoja na kazi nyinginezo.

Aidha, waziri mkuu amesema kuongezeka kwa mapato hayo kumeiwezesha serikali kuendelea kuwahudumia wananchi kupitia ujenzi na uboreshaji wa miundombinu mbalimbali kwa ajili ya shughuli za ujenzi wa uchumi na kijamii.

Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililotamatishwa na mkutano wa 18 limeahirishwa leo kwa hotuba ya waziri mkuu ambayo ndani yake imetaja kuongezeka kwa mapato ya taifa.

                                                              Mwisho.   

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.