Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Babati mkoani Manyara Yonna Keawo ametoa muda wa miezi minne, kuhakikisha fedha zote zilitotengwa na halmashauri hiyo kwa ajili ya kukamilisha baadhi ya miradi ya maendeleo iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi, zinapelekwa kwenye miradi hiyo.
Taarifa na Zacharia Mtigandi
Baadhi ya miradi hasa ya sekta ya afya katika halmashauri ya mji wa Babati iliyoanzishwa na wananchi wakitegemea kupata fedha za umaliziaji kutoka halmashauri ya mji huo haijakamilika.
Kutokukamilika kwa miradi hiyo kwa wakati ni hoja mojawapo iliyoibuliwa na madiwani katika kikao chao cha baraza.
Hoja hiyo imemsukuma mwenyekiti wa halmashauri ya mji Yonna Keawo kuagiza fedha za bajeti zilizotengwa zitumike kukamilisha miradi hiyo ndani ya miezi minne kuazia sasa.
Hoja zingine zilizoibuliwa kwenye kikao hicho cha baraza la madiwani halmshauri ya mji wa Babati ni kuhusu shule ya msingi Daraji ambayo iko hatarini kutokana na kushambuliwa na wadudu aina mchwa ambayo inahitaji kufanyiwa marekebisho.
Hata hivyo kwa mujibu wa Mkuu wa wilaya ya Babati Elizaberti Kitundu amesema ofisi yake tayari imetenga zaidi ya shilingi laki sita kusaidia ukarabati wa shule hiyo ya msingi Darajani.
Mwisho.