Mawakala inayotekeleza zoezi la usajili wa laini za simu kwa alama za vidole mkoani Njombe wameitupia lawama mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA kwa kuchelewa kukamilisha zoezi hilo kwa wakati.
Habari na Dickson Kanyika.
Zoezi la usajili wa kadi za simu kwa njia ya alama za vidole linalosimamiwa kisheria na mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA ilivyomtaka kila mmoja kuhakikisha amesajili kadi ya simu kwa mtindo huo.
Njia hii ni moja ambayo inaelezwa itasaidia mamlaka husika kudhibiti uhalifu wa kimtandao, lakini pia kuwabaini wahusika kwa urahisi zaidi pindi uhalifu wa kimtandao unapofanyika.
Imeelezwa kuwa kucheleweshwa huko kumeleta changamoto kubwa kwa wananchi ambao wanahitaji kutambuliwa laini zao za simu kwa alama za vidole, kwani wengi wao wamejikuta wakipoteza gharama nyingi kwa kusafiri kutoka vijijini hadi mijini kufuata huduma hiyo wakihofia kusitishiwa mawasiliano kama serikali ilivyowaonya kwa kuongeza muda wa siku 20 tu kutoka januari mosi hadi January 20 mwaka huu.
Baadhi ya wananchi wamesema muda uliotolewa hautoshi ukilinganisha na mwenendo wa zoezi la usajili linavyoendeshwa.
Baada ya malalamiko yote hayo ya wananchi mratibu wa NIDA mkoa wa Njombe ambapo amebainisha kuwa hakuna tatizo kwa mamlaka ya mawasiliano kuzorotesha zoezi hilo la usajili wa laini za simu kwa alama za vidole kama ambavyo raia wanailaumu mamlaka hiyo kwa kutokupata muafaka wa mawasiliano ikiwa laini zao zitazimwa.
Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA imeweza kubainisha kuwa laini ambazo hazijakamilisha usajili zitazimwa ifikapo saa sita usiku wa kuamkia January 21 mwaka huu huku wananchi walio wengi wakimlilia Rais Magufuli kuwaongezea Muda.
Mwisho.