Star Tv

Mawakala inayotekeleza zoezi la usajili wa laini za simu kwa alama za vidole mkoani Njombe wameitupia lawama mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA kwa kuchelewa kukamilisha zoezi hilo kwa wakati. 

 Habari na Dickson Kanyika.

Zoezi la usajili wa kadi za simu kwa njia ya alama za vidole linalosimamiwa kisheria na  mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA ilivyomtaka kila mmoja kuhakikisha amesajili kadi ya simu kwa mtindo huo.

Njia hii ni  moja ambayo inaelezwa itasaidia mamlaka husika kudhibiti uhalifu wa kimtandao, lakini pia kuwabaini wahusika kwa urahisi zaidi pindi uhalifu wa kimtandao unapofanyika.

Imeelezwa kuwa kucheleweshwa huko  kumeleta changamoto kubwa kwa wananchi ambao wanahitaji kutambuliwa laini zao za simu kwa alama za vidole, kwani wengi wao wamejikuta wakipoteza gharama nyingi  kwa kusafiri kutoka vijijini hadi mijini kufuata huduma hiyo wakihofia kusitishiwa mawasiliano kama serikali ilivyowaonya kwa kuongeza muda wa siku 20 tu kutoka januari mosi hadi January 20 mwaka huu.

Baadhi ya wananchi wamesema muda uliotolewa hautoshi ukilinganisha na mwenendo wa zoezi  la usajili linavyoendeshwa.

Baada ya malalamiko yote hayo ya wananchi mratibu wa NIDA mkoa wa Njombe ambapo amebainisha kuwa  hakuna tatizo kwa mamlaka ya mawasiliano kuzorotesha zoezi hilo la usajili wa laini za simu kwa alama za vidole kama ambavyo  raia wanailaumu mamlaka hiyo kwa kutokupata muafaka wa mawasiliano ikiwa laini zao zitazimwa.

Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA imeweza kubainisha kuwa laini ambazo hazijakamilisha usajili zitazimwa ifikapo saa sita usiku wa kuamkia January 21 mwaka huu huku wananchi walio wengi  wakimlilia Rais Magufuli kuwaongezea Muda.

                                                                                                               Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.