Mama mmoja aitwaye Neema Joseph mkazi wa kijiji cha Burungu wilaya ya Musoma Mkoani Mara ameliwa na Mamba wakati akioga ndani ya Ziwa Victoria majira ya saa nne usiku katika ufukwe wa Bulungu.
Habari na Sadick Hunga ...
Kamanda wa polisi mkoa wa Mara kamishina msaidizi wa jeshi la polis Daniel Shillah wakati akizungumzia tukio hilo amesema mama huyo baada ya kumaliza kufanya biashara yake ya kuuza chakula alikwenda kuoga pembezoni mwa ziwa Victoria na ndipo alipokutwa na masahibu hayo.
“Lakini katika kuoga kwenye ufukwe aliweza kukatwa na mamba na kupoetza Maisha juhudi za kutafuta mabaki ya mwili wa mama huyo zinaendelea”;ACP Daniel Shillah – Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara
Baadhi ya wakazi wa eneo wakizungumzia tukio hilo wameiomba serikali kutoa elimu juu ya ongezeko la wanyama wakali pembezoni mwa ziwa hilo na kuwaelimisha wananchi kutooga ziwani kwakuwa ni hatari endapo viumbe wa majini wa aina hiyo wanapokuwepo ndani ya maji.
Wakati hilo likijiri jeshi la polisi pia limefanikiwa kuukamata mtandao wa wauza madawa ya kulevya wanane wakiwa safarini kwenda jijini Mwanza kuyauza.
Kamanda Shillah Ametoa wito kwa wananchi kuepuka kutenda vitendo vya uhalifu kutokana na doria zinazoendelea katika maeneo mbalimbali mkoani humo.
Mwisho.