Star Tv

Mama mmoja aitwaye Neema Joseph mkazi wa kijiji cha Burungu wilaya ya Musoma Mkoani Mara ameliwa na Mamba wakati akioga ndani ya Ziwa Victoria majira ya saa nne usiku katika ufukwe wa Bulungu.

Habari na Sadick Hunga ...

Kamanda wa polisi mkoa wa Mara kamishina msaidizi wa jeshi la polis Daniel Shillah wakati akizungumzia tukio hilo amesema mama huyo baada ya kumaliza kufanya biashara yake ya kuuza chakula alikwenda kuoga pembezoni mwa ziwa Victoria na ndipo alipokutwa na masahibu hayo.

 “Lakini katika kuoga kwenye ufukwe aliweza kukatwa na mamba na kupoetza Maisha juhudi za kutafuta mabaki ya mwili wa mama huyo zinaendelea”;ACP Daniel Shillah – Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara

Baadhi ya wakazi wa eneo wakizungumzia tukio hilo wameiomba serikali kutoa elimu juu ya ongezeko la wanyama wakali pembezoni mwa ziwa hilo na kuwaelimisha wananchi kutooga ziwani kwakuwa ni hatari endapo viumbe wa majini wa aina hiyo wanapokuwepo ndani ya maji.

Wakati hilo likijiri jeshi la polisi pia  limefanikiwa kuukamata mtandao wa wauza madawa ya kulevya wanane wakiwa safarini kwenda jijini Mwanza kuyauza.

Kamanda Shillah Ametoa wito kwa wananchi kuepuka kutenda vitendo vya uhalifu kutokana na doria zinazoendelea katika maeneo mbalimbali mkoani humo.

                                                                       Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.