Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Julai, 2019 amesafiri kwa treni ya TAZARA kutoka Jijini Dar es Salaam kuelekea Kisaki Mkoani Morogoro na baadaye atakwenda Rufiji Mkoani Pwani ambako kesho atakuwa Mgeni Rasmi katika sherehe ya kuweka jiwe la msingi mradi wa kuzalisha umeme katika mto Rufiji.
Add a commentRead more: Rais; John Magufuli asafiri kwa Treni, kutoka Dar es Salaam, kuelekea Morogoro.
Halmashauri ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara imetenga zaidi ya shilingi milioni ishirini na tano ili kuwapa wakulima mbegu ili kunusuru zao la Alizeti kutokana na kiwanda cha kuongeza thamani ya zao hilo kukosa malighafi.
Add a commentSerikali imeamua kutekeleza mikakati mbalimbali yenye lengo la kuleta maendeleo kwa nchi ikiwemo sekta ya mifugo kwa lengo la kupunguza magonjwa kwa wafugaji na kuongeza uzalishaji wa maziwa na nyama kwa kupanda malisho. Wilaya zilizotembelewa ni pamoja na Maswa, bariadi pamoja na vijiji, katika mkoa wa Simiyu.
Add a commentRead more: Uhifadhi wa Malisho ya mifugo kwa njia ya Hei, DK; Mwilawa
Mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura amemweka ndani kwa muda wa saa 24 mtendaji wa kijiji cha Mau kata ya Mbulima John Ndasi baada ya kuzitafutana fedha za vitambulisho vya wajasiliamali kiasi cha shilingi milioni moja na elfu themanini.
Add a commentRead more: Mtendaji awekwa ndani kwa kula fedha za vitambulisho.
Waziri mkuu, Kassim Majaliwa amezionya Halmashauri za Wilaya na Manispaa zilizoshindwa kufikisha malengo ya makusanyo ya kodi na kuzitaka zijitathmini ni kwa nini hazijafikisha malengo hayo. Ametoa agizo hilo wakati akizungumza na washiriki wapatao 700 ambao ni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa (ALAT) unaoendelea jijini Mwanza.
Add a commentRead more: Halmashauri mapato yake hayaridhishi, Waziri Mkuu mkutano wa ALAT,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa siku 5 kuanzia leo tarehe 16 Julai, 2019 kwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Wizara ya Fedha na Mipango kuhakikisha vifaa vya ujenzi wa chelezo ya kujengea meli na vifaa vya ukarabati wa meli vilivyokwama katika Bandari ya Dar es Salaam kutokana na mchakato wa kikodi vinafikishwa katika Bandari ya Mwanza.
Add a commentTaasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU), mkoa wa Simiyu imewakamata na kuwafikisha mahakamani watendaji watatu wa serikali kwa nyakati tofauti, na hakimu wa mahakama ya mwanzo kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa.
Add a commentRead more: Watendaji wa Serikali wakamatwa kwa kuomba na kupokea Rushwa.
Moto uliozuka katika ghala la kuhifadhia pamba inayokadiliwa kuwa tani 120,000 limeteketeza pamba yote katika kijiji cha Shinyanga Mwenge kata ya Dakama wilayani Maswa mkoani Simiyu na kuwaachia kilio wakulima wa zao hilo waliouza pamba yao kwa mkopo.
Add a commentRead more: Ghala la kuhifadhia pamba lateketea kwa moto, Simiyu.
Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]
Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]
Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]
Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.