Star Tv

Halmashauri ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara imetenga zaidi ya shilingi milioni ishirini na tano ili kuwapa wakulima mbegu ili kunusuru zao la Alizeti kutokana na kiwanda cha kuongeza thamani ya zao hilo kukosa malighafi.

Serikali imewataka wawekezaji kuwekeza kwenye viwanda nchini ili viweze kuongeza  thamani ya mazao toka mashambani. Kiwanda cha kuchenjulia mafuta ya Alizeti cha Mossegi kilichopo wilayani Serengeti mkoani Mara kinakabiliwa na tatizo la ukosefu wa malighafi hatua inayoelezwa kuwatia hasara wawekezaji. Pamoja na tatizo hilo lakini pia kiwanda hicho kinatatizo la kukatika umeme mara kwa mara suala linalofanya  gharama za uendeshaji kuwa juu katika uendeshaji wake.

Kutokana na hali hiyo halmashauri ya wilaya ya Serengeti imetenga fedha zaidi ya shilling miilioni ishirini na tano ili kuweza kunusuru hali hiyo kwa kuwagawia mbegu wakulima.

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.