Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa rai kwa Serikali ya Marekani kufanya marejeo ya mkataba wa Mpango wa Ukuzaji Fursa za Kiuchumi Afrika (African Growth and Opportunity Act - AGOA) na kuuhuisha hadi mwaka 2030.

Rais Samia ametoa rai hiyo leo wakati akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kumpokea mgeni wake Mhe. Kamala Harris, Makamu wa Rais wa Marekani ambae yuko katika ziara ya kikazi nchini. Aidha, Rais Samia amesema mpango wa AGOA ambao unaisha mwaka 2025 ni muhimu kwa Tanzania kwa kuwa ni njia pekee ya biashara ambayo bara la Afrika linautegemea kujikomboa kutoka lindi la umaskini. Vile vile, Rais Samia ametoa wito kwa Marekani kufanya mapitio ya Mkataba wa Viza ili kuwawezesha raia wa mataifa yote mawili kunufaika na viza ya muda mrefu kwa kuongeza ukuaji wa biashara, utalii na uwekezaji.

Rais Samia pia ameishukuru Marekani kwa msaada wanaoutoa katika kuleta maendeleo nchini kwenye sekta za afya, elimu, maji, usafi wa mazingira, kilimo na usalama wa chakula, maliasili, maendeleo ya miundombinu, demokrasia, pamoja na utawala bora. Rais Samia amesema ziara ya Mhe. Harris itatoa fursa kwa nchi hizi mbili kuimarisha mahusiano yaliyopo na kuwa jukwaa la kutafuta maeneo mapya ya ushirikiano zaidi. Kwa upande wake, Mhe. Harris amemtaja Rais Samia kama kiongozi bingwa wa mageuzi ambapo pia amesisitiza nchi hizi zitaendelea na majadiliano juu ya ukuaji wa uchumi wa muda mrefu nchi Tanzania.

Chanzo: Ikulu Mawasiliano.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.