Star Tv

Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli amewatembelea majeruhi 43 wa ajali ya moto iliyotokea Agosti kumi mkoani Morogoro waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na kuwapatia kila mmoja Shilingili 500,000 kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Add a comment

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amekerwa na kitendo cha Mamlaka ya Maji wilayani Maswa kupandisha bili ya maji kutoka sh 5,000 hadi sh. 28,000 jambo ambalo amesema halikubaliki na amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka akutane na wahusika leo.

Add a comment

Asasi Isiyo ya kiserikali inayojihusisha na kupinga Ukatili kwa wanawake na watoto mkoani Kigoma KIWODE ikishirikina na Vyombo vya Dola na wadau wengine imezindua na kuanza kutekeleza mpango wa kupinga na kukabIlina na vitendo vya ukatili na ubakaji vinavyotajwa kuanza kuota mizizi ndani ya manispaa ya Kigoma Ujiji.

Add a comment

Mahakama ya hakimu mkazi Tarime mkoani Mara imewahukumu kifungo cha miaka 18 jela ama kulipa faini ya shilling million 315 raia kutoka nchini China kwa kukutwa na viroba tisa vyenye mchanga na boksi moja la madini wakisafirisha katika gari namba KBW 515  Toyota land Cruiser.

Add a comment

Serikali wilayani Chunya mkoani Mbeya imethibitisha kuwepo kwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili dhidi ya wanawake wakulima wawapo mashambani vinavyotekelezwa na wafugaji.

Add a comment

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Nzega Mkoani Tabora imemuagiza injinia wa Mamlaka ya Barabara mijini na vijijini Tarula kumsimamisha kazi na kukatisha mkataba wa Ujenzi kampuni ya Didia Inayojenga Daraja la Mto Nhobola baada ya kushindwa kazi.

Add a comment

Wajumbe kutoka baraza tawala la kijeshi la Sudan na muungano mkuu wa upinzani wamepiga hatua kuhusu masuala tata katika mazungumzo ya kuyahamisha madaraka kutoka utawala wa kijeshi.

Add a comment

Serikali  inaangalia njia mbadala ya ununuzi wa magari yake kwa kwenda moja kwa moja kiwandani bila kupitia kwa mawakala kutokana na gharama kuwa juu na hazitabiliki.

Add a comment

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga  ametembelea na kujionea maandalizi ya Maadhimisho ya 27 ya sikukuu ya wakulima maarufu kama (Nane Nane) yenye lengo la kuwatambua na kuwaenzi Wadau Wakuu wa Sekta ya Kilimo ambao ni Wakulima, Wafugaji, Wavuvi, Wanaushirika, Wasindikaji wa mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi na maliasili kwa mchango wao mkubwa wanaoutoa katika kuendeleza uchumi wa nchi yetu. 

Add a comment

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.