Star Tv

Jukwaa la wadau wa kilimo nchini ANSAF limefanya zoezi la ufuatiliaji wa uwajibikaji jamii wilayani Ukerewe kwa lengo la kuangalia kama michakato ya kupanga, kutekeleza na kusimamia rasilimali za umma zinafanyika kwa kuzingatia sheria na miongozo ya serikali za mitaa.

Hayo yamezungumzwa wakati wa kupokea matokeo ya uchambuzi wa ufuatiliaji na uwajibikaji jamii Huku Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Cornel Magembe, akisema ushirikishaji jamii katika shughuli za maendeleo utafungua ukurasa mpya katika Nyanja mbalimbali za maendeleo ikiwemo uvuvi. Kwa upande wake Edina Lugano kwa niaba ya mkurugenzi wa ANSAF Audax Lukonge, amesema ushirikishwaji jamii utaongeza ushawishi wa jamii kushiriki katika maswala ya maendeleo hatimaye kunufaika na rasilimali zilizopo. Jumla ya wilaya 34 nchini zimefikiwa na Jukwaa la wadau wa kilimo Tanzania ANSAF katika kuendesha zoezi la ufuatiliaji na uwajibikaji jamii ili kuongeza uwazi na uwajibikaji kwa kushirikisha jamii katika kujiletea maendeleo ambapo mambo mbalimbali ya maendeleo yamejadiliwa na kutafuta ufumbuzi wa changamoto zilizobainika.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.