Star Tv
Mwanamume aliyejibadilisha jinsia na kuwa mwanamke amefanikiwa kumyonyesha mtoto katika kisa cha kwanza cha iana yake kuwahi kushuhudiwa, watafiti wanasema. Mwanmke huyo mwenye umri wa miaka 30 alitaka kumnyonyesha mtoto baada ya mpenzi wake aliyejifungua kusema hataki kumnyonyesha mtoto huyo, hayoni kwa mujibu wa wa jarida la afya la watu waliojibadili jinsia. Alifanikiwa kunyonyesha baada ya kumeza dawa na kukamua maziwa, ripotihiyo inasema kutoka nchini Marekani. Mtaalamu wa Marekani anasema utafiti huo huenda ukachangia visa zaidi vya wanaume walijibadilisha jinsia kuwa wanawake kunyonyesha watoto. Mwanamke huyo aliyekuwa anapokea matibabu ya kubadili homoni zake mwilini kwa muda wa miaka 6, lakini hajafanyiwa upasuaji kubadili sehemu zake za siri, wakati alipowaomba madaktari wamsaidie atimize lengo lake la kumnyonyesha mtoto. Kabla ya mtoto huyo kuzaliwa, madakatari walimpadawa za miezi mitatu unusu kumsaidia kupata maziwa, kwa kawaida dawa hizo hupewa wanawake waliowaasili watoto au waliojipatia watoto kupitia wanawake wanobeba mimba kibiashara kuwaisaidia wasioweza kuzaa. Dawa hizo husisimua homoni mwilini kushinikiza kutoa maziwa na kuzuia homoni za kiume na pia alihitajika kukamua maziwa yake. Na mtokeo yake, yalimsababisha mwanamke huyo kuweza kupata maziwa kiasi. Watafiti wanasema mtoto huyo alikunywa maziwa hayo tuu kwa wiki zake sita za uhai, wakatiambapo ukuwaji wake, ulaji na uwendaji haja wake ulikuwa unaendelea kama kawaida. Baada ya hapa, mtoto alianza kupewa maziwa ya mkebe kwasababu maziwa yalianza kupungua. Mtoto huyo sasa ana miezi sita na anendelea kunyonya kama sehemu ya lishe yake, wahiriri wa utafiti huo wanasema. Add a comment
Maafisa wa polisi nchini India wamemkatama mwanamke mmoja aliyejifanya kuwa mwanamume na kuwadanganya wanawake wawili ili kulipwa mahari. Krishna Sen alikamatwa siku ya Jumatano katika jimbo la Kaskazini la Uttarakhand kwa kutaka kulipwa mahari kinyume na sheria nchini India. Maafisa wa polisi waliambia BBC kwamba iligunduliwa wakati wa mahojiano kwamba Krishna alikuwa mwanamke. Wanaamini bi Sen mwenye umri wa miaka 26 aliyejulikana kama 'sweety' amekuwa akijidai kuwa mwanamume tangu 2014 wakati alipooa kwa mara ya kwanza.Bi Sen inadaiwa aliachana na mke wake wa kwanza mara tu baada ya harusi na mke wake wa kwanza na kumuoa mwanamke mwengine mnamo mwezi Aprili 2017. Lakini mashemegi zake waliwasilisha malalamishi wakimshutumu kwa kumnyanyasa mwanao ili kulipwa mahari. Pia walidai kwamba alikuwa amewaomba takriban dola 13,297 ili kuanza biashara na kwamba hakurudisha fedha hizo. Kulipa na kukubali mahari ni utamaduni wa karne moja iliopita Kusini mwa India ambapo wazazi wa mke hulipa fedha, nguo na vito kwa familia ya mume. Ijapokuwa utamaduni huo ni kinyume na sheria nchini India tangu 1961, unaendelea. Maafisa wa polisi walisema kuwa bi Sen aliwaambia kwamba amekuwa akitaka kuwa mvulana na kuishi kama mume akiongozea haijulikani iwapo wazazi wa bi Sen walikuwa wanajua kile ambacho amekuwa akifanya. Wanawake wote aliowaoa hawakumshuku. Bi Sen hakuvua nguo mbele yao na kulingana na polisi hakushiriki nao katika tendo la ngono. Alikuwa na marafiki wa kiume, akitumia vyoo vya wanaume na kuzungumza kwa kutumia sauti tofauti , polisi wanasema. Pia alidaiwa kuvuta sigara, kunywa pombe na kuendesha pikipiki na marafikize wa kiume, ili kuondoa shauku yoyote. Akiwa amenyolewa kama mwanamume, kuvaa na kuwa na tabia za kiume Krishna alikuwa akiishi maisha ya kiume. Hakuna mtu aliyemshuku Krishina, afisa mwengine wa polisi alisema. Add a comment
Mamlaka nchini Peru zimemkamata mfungwa zaidi ya mwaka mmoja tangu atoroke jela kwa kumuacha ndugu yake pacha katika nafasi yake Alexander Delgado alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 16 wa dhuluma ya kingono kwa mtoto na wizi kwenye gereza moja kaskazini mwa Lima. Wakati ndugu yake pacha alimtembela gerezani mwezi Januari mwaka uliopita, Alexander alimwekea dawa ya kulevya, akambadilisha nguo zake na kutoroka jela. Mabadiliko hayo kwa wafungwa yalithibitiswa wakati alama za vidole za Giancarlo zilichukuliwa.Baada ya miezi 13 mafichoni Alexander Delgado alaikamatwa siku ya Jumatatu katika mji wa bandari wa Callao baada ya wizara ya masuala ya ndani kutangaza zwadi kuhusu bahari ambazo zingepelekea akamatwe. Sasa anatarajiwa kuhamishwa kwenda kwa grereza lenye ulinzi mkali kusini mwa nchi. Wakati Alexander akiwa mafichoni ndugu yake Giancarlo alikamatwa na kuchunguzwa akishukiwa kushirikiana na pacha wake. Lakini hakushtakiwa na sasa ameachiliwa. Akiongea na vyombo vya habari Alaxander Delgadoi alisema alitotoroka kwa sababu alikuwa ana hamu sana ya kumuona mama yake. Add a comment
Mwanamke mmoja wa China aliandamana na begi lake kupitia mashine ya ukaguzi ya X -Ray. Wafanyikazi katika kituo cha reli cha Kusini mwa China walishangazwa kuona mwanamke huyo akitoka ndani ya mashine hiyo pamoja na begi lake. Video moja ya mtandaoni ilionyesha kisa hicho cha kushanganza kilifanyika siku ya Jumapili baada ya kuupanda ukanda wa kusukuma mizigo. Awali mwanamke huyo alitazama begi lake likiwekwa katika mshipi huo na kuondoka.Picha za mionzi ya X-Ray zilimuonyesha mwanamke huyo akiwa amepiga magoti nyuma ya begi lake huku akiwa amevaa viatu virefu. Haijabainika ni kwa nini mwanamke huyo hakutaka kuwa mbali na begi lake ,lakini raia wengi nchini China hubeba kiwango kikubwa cha fedha wakati wanapoelekea nyumbani kusherehekea mwaka mpya. Add a comment
Nchini Ureno wamemkamata mwanamume mmoja kwenye uwanja wa ndege huko Lisbon, ambaye alikuwa amebeba kilo moja ya cocaine kwenye makalio bandia. Vyombo vya habari nchini humo vilisema kuwa raia huyo wa Brazil aliwasili kwa ndege kutoka mji wa Belém do Pará, kaskazini mwa Brazil. Haijulikani ni vipi polisi walifanikiwa kugundua hilo. Mwanamume mwingine ambaye anatuhumiwa kuwa angepokea dawa hizo alikamatwa kwenye kituo cha treni cha mji huo. Wanaume hao watakabiliwa na kesi ya ulanguzi wa madawa ya kulevya. Mwezi uliopita polisi nchini Ureno na Uhispania walikamata cocaine ndani ya mananasi yaliyokuwa yamesafirishwa kutoka Amerika ya Kusini. Add a comment

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.