Star Tv

Morocco imesema inatumia mbinu mpya katika kukabiliana na wimbi la wahamiaji wanaotaka kuitumia kama njia ya kuingilia Ulaya, na imefanikiwa kuwazuia wahamiaji 25,000 waliojaribu kuingia Uhispania kupitia njia ya Gibraltar kwa mwaka huu pekee.

Add a comment

Leo ni Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, ambapo Umoja wa Mataifa umetumia siku hii kuwatunuku waandishi wawili wa shirika la habari la Reuters wanaotumikia kifungo cha miaka saba nchini Myanmar tuzo ya juu kabisa ya uhuru wa vyombo vya habari.

Add a comment

Raia wa Ukraine wanapiga kura leo katika uchaguzi ambao unaweza kushuhudia msanii wa vichekesho ambaye hajawahi kushika wadhifa wowote wa kisiasa akichaguliwa kuwa rais.

Add a comment

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameahidi kulijenga upya kanisa kuu Katoliki la Notre Dame mjini Paris ambalo liliungua moto jana jioni na kusababisha uharibifu katika sehemu ya jengo hilo. Kanisa la Notre Dame lilijengwa karne ya 12 na limekuwa ni mojawapo ya vivutio vya utalii nchini Ufaransa. Kanisa hilo lilikuwa chini ya ukarabati ambao umetajwa na vyombo vya habari vya ndani kuwa chanzo cha moto. Moto huo umeunguza na kuangusha mnara wa juu wa kanisa ulio na urefu wa mita 93 ambao umekuwa ni alama ya utambulisho, lakini mkuu wa kikosi cha Zimamoto Jean-Claude Gallet amesema sehemu kubwa ya Kanisa imeweza kuokolewa baada ya maafisa kuzuia moto kuenea zaidi. Viongozi mbalimbali ulimwenguni wametuma salamu za pole kutokana na mkasa huo ambapo Kansela Angela Merkel amelielezea kanisa hilo kuwa ishara ya Ufaransa na utamaduni wa Ulaya.

CHANZO: Idhaa ya kiswahili ya DW

Add a comment

Mkuu wa majeshi nchini Algeria ametaka rais wa nchi hiyo mwenye umri wa miaka 82, Abdelaziz Bouteflika atangazwe kuwa hana uwezo wa kuongoza nchi. Mkuu huyo wa majeshi Ahmed Gaid Salah amesema Bouteflika anaweza kuondolewa madarakani kwa mujibu wa katiba.

Add a comment

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.