Morocco imesema inatumia mbinu mpya katika kukabiliana na wimbi la wahamiaji wanaotaka kuitumia kama njia ya kuingilia Ulaya, na imefanikiwa kuwazuia wahamiaji 25,000 waliojaribu kuingia Uhispania kupitia njia ya Gibraltar kwa mwaka huu pekee.
Ingawa haikuelezea zaidi ni teknolojia gani wanayoitumia, lakini mkuu wa usalama wa mipakani wa Morocco, Khalid Zerouali, amesema kwenye mahojiano na shirika la habari la Associated Press kwamba teknolojia ya ufuatiliaji na vikosi imara kwa pamoja vimesaidia kuimarisha usimamizi. Zerouali amesema mafanikio hayo ni asilimia 30 zaidi, ikilinganishwa na mwaka jana ya kuwazuia wahamiaji kupitia Gibraltar kuingia Uhispania, na hususan kati ya miezi ya Februari na Aprili.
CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW