Asasi Isiyo ya kiserikali inayojihusisha na kupinga Ukatili kwa wanawake na watoto mkoani Kigoma KIWODE ikishirikina na Vyombo vya Dola na wadau wengine imezindua na kuanza kutekeleza mpango wa kupinga na kukabIlina na vitendo vya ukatili na ubakaji vinavyotajwa kuanza kuota mizizi ndani ya manispaa ya Kigoma Ujiji.
Vitendo hivyo vimekuwa vikihusishwa na imani za kishirikina. Mkakati huu unahusisha ,jeshi la polisi ,Viongozi wa Serikali za mitaa viongozi wa Dini na wananchi wa kawaida unatarajiwa kuwa chachu ya kuyabaini maeneo
na watu wanaoendesha vitendo hivyo na kufikishwa katika mamlaka za kisheria.Jeshi la Polisi limeahidi kutoa ushirikiano mkubwa katika suala hilo, huku idara ya maendeleo ya jamii manispaa ya kigoma katika mpango huo ikijikita katika suala la uelimishaji umma. Kata zinazotajwa kukithiri kwa vitendo vya aina hiyo ya ubakaji ambako mpango huo utaanza kutekelezwa ni, Bangwe, Mwanga kaskazini, Kibirizi, Matubukana na Mwanga kusini.