Star Tv

Asasi Isiyo ya kiserikali inayojihusisha na kupinga Ukatili kwa wanawake na watoto mkoani Kigoma KIWODE ikishirikina na Vyombo vya Dola na wadau wengine imezindua na kuanza kutekeleza mpango wa kupinga na kukabIlina na vitendo vya ukatili na ubakaji vinavyotajwa kuanza kuota mizizi ndani ya manispaa ya Kigoma Ujiji.

Vitendo hivyo vimekuwa vikihusishwa na imani za kishirikina. Mkakati huu unahusisha ,jeshi la polisi ,Viongozi wa Serikali za mitaa viongozi wa Dini na wananchi wa kawaida unatarajiwa kuwa chachu ya kuyabaini maeneo
na watu wanaoendesha vitendo hivyo na kufikishwa katika mamlaka za kisheria.Jeshi la Polisi limeahidi kutoa ushirikiano mkubwa katika suala hilo, huku idara ya maendeleo ya jamii manispaa ya kigoma katika mpango huo ikijikita katika suala la uelimishaji umma. Kata zinazotajwa kukithiri kwa vitendo vya aina hiyo ya ubakaji ambako mpango huo utaanza kutekelezwa ni, Bangwe, Mwanga kaskazini, Kibirizi, Matubukana na Mwanga kusini.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.