Star Tv

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Nzega Mkoani Tabora imemuagiza injinia wa Mamlaka ya Barabara mijini na vijijini Tarula kumsimamisha kazi na kukatisha mkataba wa Ujenzi kampuni ya Didia Inayojenga Daraja la Mto Nhobola baada ya kushindwa kazi.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Mkuu wa wilaya ya Nzega Godfrey Ngupulla amesema mkandarasi huyo ameshindwa kufanya kazi kutokana na mkataba kumtaka kuanzi kazi mwezi Januari 2019 na kumaliza Julai 2019 lakini hakuna kazi yoyote iliyofanyika.

Ameongoza, Daraja hilo ni miongoni mwa ahadi za Mh,Rais Dk;John Pombe Magufuli dhidi ya wananchi wa Kijiji cha Nhobola ambao wamekuwa wakipata adha ya kuvuka nyakati za mvua za masika hali ambayo hugeuka kijiji hicho kuwa kisiwa.

Amemuagiza Injinia wa Tarula mkoa wa Tabora Regnard Silanga kumtoa mkandarasi huyo kisha kutangaza tenda ili apatikane mkandarasi mwingine atakayeweza kujenga Daraja hilo kwa muda uliopangwa.Daraja hilo lilitengewa shilingi milioni 440 za ujenzi pamoja na kukarabati barabara ili wananchi hao wafanye shughuli zao za maendeleo pamoja na kuondokana na usumbufu. Mkandarasi huyo tayari amesimamishwa na mchakato wa kumpata mkandarasi mwingine unaendelea ili akamilishe ujenzi huo ambao ni hitaji la wananchi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.