Star Tv

Mtoto aitwaye Veronica Anthony mwenye umri wa miaka 17,Mwanafunzi wa darasa la saba wa Shule ya msingi Kayenze ambaye ni mkazi wa Iseni amefariki dunia kwa kupigwa na kitu kizito kichwani.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Muliro Jumanne Muliro, ametoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari leo Septemba 10,2020, Ambapo amebainisha kuwa;
"Tarehe 08.09 2020 Majira ya saa nne usiku maeneo ya Kata ya Kayenze wilayani Ilemela baba alimuua binti yake kwa kumpiga na kitu kizito kichwani kwa kosa la kuchelewa kurudi nyumbani, kitendo kilichomkasrisha baba yake mzazi".

Aidha, Kamanda Muliro amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa uchunguzi wa Daktari, huku mtuhumiwa ambaye ni baba mzazi aliyejulikana kwa jina la Constatine Maningu tayari amekamatwa na atafikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.