Mtoto aitwaye Veronica Anthony mwenye umri wa miaka 17,Mwanafunzi wa darasa la saba wa Shule ya msingi Kayenze ambaye ni mkazi wa Iseni amefariki dunia kwa kupigwa na kitu kizito kichwani.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Muliro Jumanne Muliro, ametoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari leo Septemba 10,2020, Ambapo amebainisha kuwa;
"Tarehe 08.09 2020 Majira ya saa nne usiku maeneo ya Kata ya Kayenze wilayani Ilemela baba alimuua binti yake kwa kumpiga na kitu kizito kichwani kwa kosa la kuchelewa kurudi nyumbani, kitendo kilichomkasrisha baba yake mzazi".
Aidha, Kamanda Muliro amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa uchunguzi wa Daktari, huku mtuhumiwa ambaye ni baba mzazi aliyejulikana kwa jina la Constatine Maningu tayari amekamatwa na atafikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria.