Kwa mara ya kwanza katika historia, rais wa Gabon, Ali Bongo, amemteua mwanamke, Christiane Ossouka Raponda kuhudumu kama waziri mkuu katika serikali. Ni mwanamke wa kwanza kuteuliwa kwenye nafasi hiyo, baada ya miaka 60 baada ya uhuru wa nchi hiyo.
Rose Christiane Ossouka Raponda (56), sio maarufu nchini Gabon Na ni mwanamke wa kwanza kuteuliwa kama Waziri Mkuu, pia alikuwa mawanamke wa kwanza kuchaguliwa kuwa meya wa mji wa Libreville mnamo mwaka 2014.
Hata hivyo mwaka 2019, Rais Ali Bongo alimtengua kwenye wadhifa wake na kumteua kuwa waziri wa Ulinzi, wadhifa ambao alikuwa akishikilia hadi baada ya uteuzi wake kama Waziri Mkuu wa Gabon.
Rose Christiane Ossouka Raponda aliingia kwa mara ya kwanza madarakani mnamo 2012, Pia Rais Bongo alimteua kuwa Waziri wake wa Bajeti wadhifa uliomstahili, kwa sababu Rose Christiane Ossouka Raponda ni mchumi. ambaye amehitimu katika Chuo Kikuu cha Uchumi na Fedha nchini Gabon.
Wataalamuwa masuala ya siasa nchini Gabon wanasema kazi yake kubwa kama Waziri Mkuu itakuwa ni kufufua uchumi na labda kufanya maandalizi ya uchaguzi ujao wa urais uliopangwa kufanyika mwaka 2023.