Star Tv

Serikali imepanga kuweka utaratibu wa kisheria utakaowataka wawekezaji wa Viwanda,Mazao, Bidhaa na Huduma kutotumia nguvu ya soko kuwakandamiza wateja.

Kauli hiyo ya serikali imetolewa bungeni leo Mei 05, 2020 jijini Dodoma na Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa Bungeni wakati akiliwasilisha bajeti ya Wizara yake kwa Mwaka wa fedha 2020/2021.

Waziri Bashungwa amesema Wizara anayoiongoza imeweka malengo na mikakati madhubuti yakuhakikisha soko la uhakika nje ya nchi linakwenda vyema na bidhaa za Tanzania zinapasua mawimbi ndani na nje ya nchi.

Kilio cha Kamati ya kudumu ya Bunge inayoshughulika na Viwanda, Biashara na Mazingira kwa muda mrefu ni mwenendo usioridhisha wa utoaji wa fedha za miradi ya maendeleo na baadhi ya Wabunge wameomba fedha zinazoombwa kwenye Wizara hiyo ni vyema zikatolewa mapema pasipo ubabaishaji ili kuendeleza Viwandana kuleta matokeo chanya kwa taifa.

Bunge limepitisha shilingi Bilioni 81. 36 ili Wiizara ya Viwanda na Biashara iweze kutekeleza majukumu yake kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.