Mbunge wa jimbo la Sumve maarufu kama Seneta kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Richard Mganga Ndassa amefariki dunia leo Aprili 29, 2020.
Kifo cha Mbunge Ndassa kimetangazwa na Spika wa Bunge Mhe.Job Ndugai ambapo mbunge huyo amefikwa na umauti leo jijini Dodoma alikokuwa akipatiwa matibabu.
Mbunge Ndassa alikuwa bungeni kwa siku nyingi ambapo amekuwa bungeni kwa miaka 25, ambapo aliliongoza jimbo la Sumve lililoko mkoani Mwanza kwa vipindi vitano ambavyo ni (1995/2000, 2000/2005, 2005/2010, 2010/2015, na 2015/2020).