Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ametoa taarifa ya mwenendo wa Ugonjwa wa Corona nchini leo Aprili 29,2020, ambapo amesema kuwa kuna maambukizi mapya ya ugonjwa huo kwa Watanzania 196.
Katika visa hivyo 196 watu 174 wanatoka Bara na kwa upande wa Zanzibar wamepatikana 22 ambao wamefanya idadi ya Watanzania waliopata maambukizi ya ugonjwa huo kufikia 480.
Aidha amesema kuwa idadi ya wagonjwa waliopona imeongezeka kutoka 48 hadi kufikia 167, (Ambapo Zanzibar wagonjwa 36 wamepona, na kwa upande wa Bara wagonjwa 83 wamepona na kuruhusiwa kutoka hospitalini.
Waziri Majaliwa amesema vifo 6 vimetokea ambavyo vimefanya jumla ya waliofariki kwa ugonjwa wa Corona kufikia 16 hadi sasa.