Star Tv

Wizara ya Afya ya Zanzibar imetoa taarifa ya mwenendo wa Corona nchini leo Aprili 28, 2020 ambapo watu 7 ambao ni raia wa Tanzania kutokea Unguja wamekutwa na maambukizi ya Virusi vya Corona.

Visa vya wagonjwa 7 vilivyotajwa leo kuongezeka vimefikisha  idadi ya wagonjwa kuwa 105 kutoka 98 ambao walitolewa taarifa tarehe 24 Aprili, 2020.

Wizara imesema imewaruhusu wagonjwa 36 kwenda nyumbani baada ya dalili zao za maradhi kuondoka ikiwemo homa, kikohozi, kifua kubaba na kuumwa kichwa.

mbali na wagonjwa hao kuruhusiwa kutoka wameshauriwa na wataalamu wa Afya kubaki katika nyumba zao kwa muda wa siku 14 na kuahidiwa kuendelea kufuatiliwa kwa karibu na wataalamu hao ili kujionea maendeleo yao pindi wawapo nyumbani.

Serikali ya visiwani humo imewataka wananchi wake kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo wa Corona na pia imewataka wananchi ambao wana dalili za homa kali, kukohoa na kupiga chafya kuweza kujitokeza katika vituo vya afya mapema au kupiga simu namba 190.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.