Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ametoa taarifa juu ya uwepo wa ongezeko la visa vipya 53 vya ugonjwa wa corona nchini tarifa iliyoongeza idadi ya watu walioathirika na ugonjwa huo kufikia 147.
Waziri Ummy akiongea na vyombo vya habari leo Aprili 17,2020, amesema wagonjwa wote hao ni watanzania ambapo 38 ni kutoka Dar es Salaam,10 Zanzibar, Kilimanjaro 1, Mwanza 1, Pwani 1, Lindi ,na Kagera 1.
Waziri Ummy amesema mgonjwa mmoja amefariki dunia na hivyo kufanya idadi ya waliofariki hadi sasa kufika 05 na waliopona ni 11.