Star Tv

Waziri wa Wizara ya Afya Ummy Mwalimu ametangaza kuwepo kwa ongezeko la visa 14 vipya vya wagonjwa wa corona nchini leo Aprili 13,2010.

Waziri ummy amesema wagonjwa wote 14 ni raia wa Tanzania na mpaka kufikia sasa idadi ya watu 46 wameambukizwa virusi vya corona.

Watu 13 kati ya walioambukizwa virusi vya corona wamepatikana jijini Dar es Salaam huku mwingine mmoja akitokea jijini Arusha.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na wizara ya afya leo asubuhi imebainisha kuwa wagonjwa wote wanaendelea na matibabu chini ya uangalizi wa wataalamu wa afya.


Ikumbukwe kuwa ni jana tu   Aprili 12, 2020 mamlaka ya usafiri wa anga nchini Tanzania TCAA ilitangaza marufuku ya ndege za abiria za kimataifa kutua nchini, Na tangazo hilo  lilibainisha kuwa rubani na wahudumu wa ndege hizo watatakiwa kukaa karantini katika maeneo yaliyotengwa na serikali kwa gharama zao binafsi.

          

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.