Star Tv

Waziri wa Afya nchini Ummy Mwalimu amesema kuwa mgonjwa mwingine aliyekuwa na maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19) nchini amepona.

Waziri Ummy ametoa taarifa hiyo leo Ijumaa Aprili 03, 2020 kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii ikiwemo akaunti ya Twitter ana Instagram.

Amesema kuwa mgonjwa huyo alikuwa Ngara mkoani Kagera amepona na kupona kwakwe mgonjwa huyo kunafikisha idadi ya waliopona Corona kuwa watatu.

Pia Waziri Ummy pia ameandika kupitia kurasa zake hizo kuwa “Mgonjwa aliyebaki Arusha vipimo vyake siku ya 9 leo ni Negative, Tutampima siku ya 14 ili kujiridhisha kama amepona. Wagonjwa wengine 15 waliobaki wanaendelea vizuri”.

Waziri Ummy ameendelea toa rai na kusisitiza wananchi kuendelea kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa huo kwa kuepuka misongamano , mikusanyiko safari zisizo za lazima na pia kufuata maelekezo ya wataalam ili kujikinga na maambukizi ya COVID-19

                                           Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.