Star Tv

Watumishi watano wa Shirika la Reli Tanzania TRC wamefariki kwa ajali ya treni ya uokoaji iliyogongana na Kiberenge Na. HDT-3 katika eneo lililopo kati ya Stesheni ya Mwakinyumbi na Gendagenda katika reli inayotoka Ruvu Junction mpaka Mruanzi Junction, tarehe 22 Machi 2020.

Taarifa hiyo imetolewa leo  katika vyombo vya habari na Jamila Mbarouk ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Habari na Uhusiano TRC imethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo imegharimu Maisha ya wafanyakazi wake watano.

Ajali hiyo imehusisha watumishi sita wa TRC ambapo watumishi wane walifariki eneo la ajali na majeruhi wawili walifikishwa katika Hospitali ya Wilaya ya (Magunga) iliyopo Korogwe mkoani Tanga kwa ajili ya huduma za kitabibu, ilipofikia saa tano usiku (23:00) tarehe 22 Machi 2020 majeruhi mmoja alifariki na kufikisha jumla ya vifo vya watumishi watano katika ajali hiyo.

Watumishi waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni; Ramadhani Gumbo ambaye alikuwa ni Meneja Usafirishaji Kanda ya Tanga, Eng. Fabiola Moshi ambaye alikuwa Meneja Ukarabati wa Mabehewa ya abiria kanda ya Dar es Salaam, Joseph Komba aliyekuwa Meneja Msaidizi Usafirishaji Kanda ya Dar es Salaam, Philibert M. Kajuna; Mtaalamu wa Usalama wa Reli pamoja na George Urio ambaye alikuwa dereva wa Kiberenge

Mpaka sasa aliyejeruhiwa ni mtu mmoja ambaye ni Elizabeth Bona aliyekuwa muongoza treni anaendelea na matibabu.

Jamila ameeleza kuwa uchunguzi wa kujumuisha kwa kushirikiana na taasisi nyingine utafanywa ili kubaini chanzo cha ajali hiyo ambacho mpaka sasa hakijajulikana, na amsema taarifa zaidi zitaendelea kutolewa kuhusu maandalizi ya kuhifadhi miili ya watumishi hao.

Mwisho.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.