Star Tv

Chama cha Mapinduzi CCM kimesitisha shughuli zenye mikusanyiko ya watu wengi ikiwa ni hatua za kudhibiti kuenea kwa virusi vya Corona.

Ugonjwa huo ulioanzia katika mji wa Wuhan, China Desemba, 2019 na baadaye kuanza kusambaa nchi mbalimbali umesababisha vifo vya watu zaidi ya 4,500 huku Tanzania ikiwa nchi ya tatu Afrika Mashariki kuwa na mgonjwa wa corona baada ya Kenya na Rwanda.

Agizo hilo na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Kwa upande mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia ameshauri vyama vya siasa nchini Tanzania kusitisha mipango ya kuendesha mikutano ya hadhara ili kupunguza tishio la kusambaa virusi vya corona.

Mbatia ameshauri Serikali kuhakikisha inatoa mwongozo na taarifa mara kwa mara kuhusu hali ya ugonjwa huo pamoja na kuongeza elimu ya uraia kwa raia wanaoendelea kukusanyika.

Mbatia ametoa ushauri huo jijini Dar es salaam ikiwa ni siku moja baada ya Wizara ya Afya kutangaza rasmi kuingia kwa ugonjwa huo nchini, Mbatia ambaye ni mbunge wa Vunjo amesema tayari ameanza kuchukua tahadhatri hiyo baada ya kisitisha ziara yake Machi 21, mwaka huu katika kata 16 za jimbo hilo. 

              Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.