Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli leo Machi 16, 2020 amefuta mbio za Mwenge kwa mwaka huu 2020 hadi pale ugonjwa wa corona utakapoisha.

Rais Magufuli amesema ameamua kufuta mbio hizo mwaka huu  kwa kuwa zinaleta mkusanyiko wa watu wengi na kutokana na ugonjwa wa corona unaoendelea kuongeza idadi ya wagonjwa kila kukicha na hata kusababisha vifo, kuwepo kwa mbio hizo kutahatarisha maisha ya watanzania wengi.

Kwa mwaka huu mbio za mwenge zilitegemewa kuwashwa Zanzibar hivi karibuni  ambapo ungewezwa kutembezwa nchi nzima na kwa kuchukua tahadhari ya ugonjwa huo ni vyema kuchukua tahadhari mapema zakuzuia mikusanyiko.

Rais Magufuli amesema fedha za mwenge ambazo zilipaswa kutumika kuwasha mwenge Zanzibar zitatumika katika kujiandaa na tahadhari zaidi ya corona ambayo kwa sasa tayari imeshafika Kenya na Rwanda.

 “Ndugu zangu ugonjwa huu unaua,ugonjwa ushafika kwa majirani zetu ni lazima  tuchukue tahadhari utatumaliza”-amesema Rais Magufuli.

Amesema hadi sasa hakuna mgonjwa wa corona hapa nchini na mbio za mwenge zitaendelea itakapothibitishwa ugonjwa huo umeisha duniani.

Aidha, Rais Magufuli ameendelea na ziara katika barabara zinazoendelea na ujenzi wa kupanuliwa ambazo ni za Mwenge, Mbezi na Kimara huku aikisisitiza wananchi kuchukua tahadhari na kuwatahadharisha watanzania kutokugusana na kuepuka misongamano.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi mtendaji wa Wakala wa Barabara (Tanroads), Patrick Mfugale amesema ujenzi wa daraja la Mfugale  linalounganisha barabara ya Morogoro, Mandela na Sam Nujoma umefikia zaidi ya asilimia 70.

Patrick amesema ujenzi wa daraja hilo unatumia zaidi ya Shilingi bilioni 200 huku Rais Magufuli akipongeza maendeleo mazuri ya ujenzi wa daraja hilo kwa kusema ameridhishwa na  ujenzi huo.

          Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.