Star Tv

Wakazi wa Vijiji vya Shimbi na letu Wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro wameeleza kukumbana ya upatikanaji wa huduma ya maji inayowalazimu kutembea hadi nchi jirani ya Kenya baada ya mradi wa maji unaotekelezwa kwenye eneo hilo kuchukua zaidi ya miaka saba bila kukamilika.

Habari na Rodrick Mushi

Wakizungumza mbele ya Naibu Waiziri wa maji Juma Aweso wamesema kuwa licha ya ahadi ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu kuagiza mradi huo ukamilike mwezi machi mwaka jana lakini hadi sasa haujakamilika huku wananchi  hao wakiendeleaa kutaabika kupata huduma ya maji..

Baada ya kutoridhishwa na utekelezaji wa mradi huo ambao umekwama kwa miaka saba Naibu Waziri wa maji Juma Aweso ameagiza msimamizi Godson Josea na Mhandisi Amosi Thomas wanaotekeleza mradi wa maji wa kijiji cha shimbi kushikiliwa na jeshi la polisi na kuagiza kusimamishwa kuendelea na ujenzi wa mradi huo.

Wasimamizi wa mradi ambao wanashikiliwa na jeshi la polisi wametakiwa kukaa rumande hadi mkandarasi aliyepewa mradi huo atakapoonana na uongozi wa wilaya.

                                                                                                             Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.