Mahakama ya Hakimu mkazi mkoa wa Njombe imeendelea kusikiliza kesi inayomkabili Mwalimu Focus Mbilinyi anayekabiliwa na tuhuma za kumpiga mwanafunzi na kumsababishia.
Habari Zaidi na Dickson Kanyika
Shauri hilo namba 141 la mwaka 2019 linaloendeshwa na Hakimu Ivran Msaki mbele ya mawakili wasomi Elizabeth Malya upande wa serikali huku upande wa utetezi ukiongozwa na mawakili Octavian Mbugwani , Innocent Kibadu na Lilian Gama limeendelea kusikilizwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa njombe.
Mahakama imewasikiliza mashahidi wawili wa upande wa utetezi ambao wote wameiambia mahakama kwamba Hosea alipigwa viboko vitatu sehemu za makalio kwa kosa la kutofanya hesabu alizopewa na mwalimu wake.
Mmoja wa mashahidi hao Sefania Kyelula ameiambia mahakama kwamba siku ya tarehe 21 mwezi machi mwaka 2017 Hosea Manga alipowasili shuleni alimueleza kwamba alikuwa akisumbuliwa na miguu kabla ya kupigwa na kusababishiwa ulemavu.
Mashahidi wote wawili wameiambia mahakama kwamba Hosea Manga hakuning’inizwa dirishani kama ilivyoelezwa hapo awali na mashahidi wa upande wa jamhuri.
Mwalimu Focus Mbilinyi anadaiwa kumpiga mwanafunzi Hosea na kumsababishia ulemavu siku ya tarehe 21 mwezi machi mwaka 2017.
Mahakama imeahirisha kesi hiyo hadi tarehe 4 mwezi February mwaka huu itakaposikilizwa tena kwa ajili ya majumuisho na kutajwa tarehe ya hukumu.
Mwisho.