Star Tv

Tume ya Vyuo Vikuu nchini TCU imefuta hati za usajili wa vyuo vikuu vishiriki vitano, vyuo vikuu vitatu na chuo kikuu kishiriki kimoja baada ya kushindwa kufanya maboresho waliyopewa kwa zaidi ya miaka mitatu.

Taarifa zaidi na Angella Mathayo.

Hayo yamesemwa na katibu mtendaji wa TCU  Profesa Charles Kihampa wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, ambapo ameeleza kuwa vyuo hivyo vimeshindwa kujirekebisha na hata vingepewa muda zaidi visingeweza.

Katika hatua nyingine TCU imefuta hati za usajili za vyuo vikuu vitatu na chuo kikuu kishiriki kimoja baada ya baada ya kushindwa kufanya maboresho kwa muda waliopewa ikiwa ni pamoja na uhaba wa rasilimali fedha katika kujiendesha.

TCU imerejesha udahili wa wanafunzi wapya katika chuo kikuu kishiriki cha afya na sayansi shirikishi cha Mt. Fransisko baaada ya kurekebisha mapungufu yaliyokuwepo.

Aidha, TCU imesitisha udahili wa wanafunzi wapya wa chuo kikuu cha kumbukumbu ya Sebastian Kolowa ambapo chuo hicho kimepewa miezi sita  kuweza kukamilisha utekelezaji wa maelekezo ya tume.

                                                                                        Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.