Star Tv

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza ACP Muliro Jumanne amekanusha taarifa zilizokuwa zinasambaa katika mitandao ya kijamii zikieleza kuwa kuna wanachama hao wa CHADEMA wametekwa jijini Mwanza.

Muliro amesema hakuna utekaji uliotokea bali wanachama hao walikamatwa na jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema wa mtaa wa Mahina.

Kamanda Muliro, akizungumza na waandishi wa habari amesema baada ya kupatikana taarifa zilizokuwa zibainisha kuwa siku ya Disemba 29, Mwaka huu Majira ya 15:00 mtaa wa Mahina Kata ya Mahina wilayani Nyamagana kulipatikana taarifa toka kwa raia wema kuwa kumeonekana watu wawili waliohisiwa kuwa siyo watu wema wakiwa karibu na Hoteli ya Paradise.

“Jeshi la polisi  lilifanya ufuatiliaji wa haraka na kufika eneo hilo na kuwakamata watu hao wawili, ambao katika mahojiano ya awali walikataa kutoa utambulisho wao kuwa wamefika maeneo hayo kufanya shughuli gani”, Amesema ACP Muliro.

Amesema baada ya wanachama hao kukamatwa walichukuliwa na kupelekwa kituo cha polisi cha kati na kutoa ushirikiano kwa askari pia kutaja majina yao kuwa ni Abdukarimu Muro (31),  ambaye ni afisa habari wa katibu mkuu CHADEMA Mkazi wa Kinondoni B, Dar es Salaam na Said Haidani (30), Dereva wa katibu mkuu CHADEMA, Mkazi wa Mbezi Kimara Dar es Salaam wameambatana na Katibu Mkuu CHADEMA, Mh. John Mnyika pamoja  na polisi waliwaachia huru baada ya kujiridhisha hawakuwa wahalifu.

Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza limetoa onyo kwa  watu wasiokuwa na taarifa rasmi na wenye tabia ya kuzusha mambo hasa  watu wanapokamatwa kwa kusema wametekwa waache tabia hiyo.

Aidha,amesema hali hiyo yakutoa taharuki ininazusha taharuki kwa jamii na kwa kufanya hivyo ni makosa na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao pindi  watakapobainika.

 

 Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.