Star Tv

Naibu waziri wa Nishati Subira Mgalu amemuagiza Meneja wa Shirika la Umeme nchini TANESCO mkoa wa Pwani Martin Maduu kuangalia namna ya kuwaunganishia umeme wananchi wanaokuwa wametoa nusu ya fedha zao ili waweze kukatwa wakati wa kununua luku na hivyo kuanza kunufaika mapema badala ya kusubiri hadi wanapomaliza kulipia.

 

Naibu waziri Mgalu amewasha Umeme katika Kijiji cha Migudeni Kata ya Kiromo wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani ambapo Umeme huo utasaidia kusukuma maji katika kisima kilichopo na wakazi wa hapo kunufaika na Umeme.

 

Aidha Mgalu amekabidhi Cement mifuko 50 kwaajili ya Ujenzi wa shule ya msingi kiromo ambayo ni shule mpya.

 

Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Shukuru Kawambwa amemshukuru Naibu waziri pamoja na waziri wa kwa kusimamia masuala ya Umeme Tanzania nzima na hasa mkoa wa Pwani.

 

                                                                     Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.