Star Tv

Mamlaka ya usafiri wa anga Tanzania TCAA imewataka wanafunzi kusoma masomo ya sayansi ili kutatua changamoto ya upungufu wa marubani nchini.

Rai hiyo imetolewa wakati Tanzania ikiungana na nchi nyingine kuadhimisha siku ya kimataifa ya usafiri wa anga duniani.

Taarifa na Adam Damian

Zoezi la kupandisha bendera ya shirika la kimataifa la usafiri wa anga duniani ICAO ambalo limetimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake ikiwa ni ishara ya kutekeleza matawaka ya shirika hilo lililoagiza kupandishwa bendera hiyo katika mlima Kilimanjaro

Kaimu mkurugenzi mkuu TCAA Vallery Chamlungu amesema Tanzania bado haina marubani wa kutosha na kwamba mamlaka ya usafiriki wa anga imeitumia siku hiyo kuwataka wanafunzi kupenda masomo ya sayansi

Baaadhi ya wanafunzi walioshirki kwenye maadhimisho hayo wamesema watahakikisha wanafanya juu chini ili kuchangamkia fursa hiyo huku wakiishukuru TCAA kwa kuanzisha vilabu mashuleni kwani zinawasaidia kupata elimu ya masuala yanayohusu  usafiri wa anga

Aidha TCAA imesema itahakikisha anga la Tanzania linaendelea kuwa salama zaidi kwa kufunga rada na mitambo ya kisasa ya kuongozea ndege sambamba na kuwasomesha wataalam wake ili waweze kuongeza ufanisi zaid katika huduma za usafiri wa anga

Katika hatua nyinge TCAA imewatunuku zawadi washindi watano wa insha iliyowataka waeleze mchango wa shirkika la ndege nchini ATCL katika uchumi wa nchi iliyowahusisha wanafunzi wa shule mbalimbali nchini

Maadhimisho ya kimataifa ya usafiri wa anga duniani yamebeba kauli mbiu isemayo miaka 75 ya kuunganisha dunia’ 

 

                                                                                       Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.