Star Tv

Anguko la baadhi ya benki nchini limetajwa kusababishwa na masharti magumu ya uendeshaji wa taasisi za kifedha yaliyowekwa na benki kuu “BoT” likiwemo sharti la kianzio cha mtaji linalodaiwa kuzipa wakati mgumu benki za wananchi kupata leseni ya kufanya kazi.

 Taarifa na Oliver Motto:-

Wanahisa wanaomiliki benki ya wananchi Mucoba PLC – wamesema kufa kwa benki nyingi za wananchi sababu ni masharti magumu yaliyowekwa na benki kuu “BoT” likiwemo sharti la benki za kijamii kuwa na mtaji usiopungua kiasi cha shilingi Bilioni mbili - jambo linalotazamwa na wanahisa kama ni miongoni mwa vikwazo kwa benki zao

Wananchi Wilayani Mufindi kwa kiwango kikubwa ndiyo wametajwa kuwa waanzilishi na wamiliki wa Benki ya wananchi Mucoba – benki ya kijamii inayoendeshwa kwa hisa za wakulima na wafanyabiashara wadogo na wakati, wananchi hao wameiomba benki ya BoT iwapunguze masharti ili benki za wananchi ziweze kuendelea.

Omary Msuya ambaye ni  afisa wa benki kuu - dawati la BoT lililopo katika benki ya Mucoba, ametoa ufafanuzi juu ya hili kwa kusema kuwa.“Baada ya vitu kukaa  sawa na mipangilio yote haya yote yatatatuliwa na gawio mtaweza kulipata hivyo muwe wavumilivu”.Anasema Omari Msuya

Haya yote yamezungumzwa na wanahisa katika mkutano mkuu wa 20 wa mwaka 2019 uliofanyika Mafinga Wilayani Mufindi- ambapo wanahisa walikwama kupata gawio kwa madai ya zuio lililowekwa na BoT.

 

                                                                                                  Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.