Wakazi wa kijiji cha Pemba wilayani Mvomero Mkoani Morogoro wamewataka viongozi wakiwemo Mbunge na Diwani kujitathimini kutokana na viongozi hao kutajwa kushindwa kutatua tatizo sugu la ubovu wa barabara ambayo ni kikwazo cha kusafirisha mazao yao na kufanya kuozea mashambani.
Ni Safari ya kuelekea kjiji cha Pemba, kijiji ambacho kipo wilayani Mvomero mkaoni hapa, usafiri unaotumika kwa sasa kufikia kijijini hapo ni usafiri wa pikipiki ambao nao unahitaji umakini wa dereva ili kuweza kufika salama.
Ubovu wa Miundombinu unahakisi maisha halisi ya watu wa kijiji cha pemba, ambao wao wanaona usimamizi mbovu wa viongozi wao ndio unachangia wao kuishi katika hali ngumi na kushindwa kusafirisha mazao yao.
Kijiji hicho kinatajwa kushika nafasi ya Pili kwa kuingizia mapato halmashauri ya wilaya ya Mvomero kutokana na uzalishaji kwa mazao kwa wingi ikiwemo miwa, Kahawa na magimbi
Niliweza kuwatafuta viongozi hao wawili kwa njia ya simu ya mkononi akiwemo mbunge na diwani wa kata hiyo lakini niliweza kufanikiwa kumpata tu diwani ndugu Kimaisi Palasino kujibu tuhuma hizo za wananchi ambaye naye bila kusita anasema mambo hayo yanatokana na siasa na sio barabara pekee..
Tatizo hili limeathiri sio tu Maisha ya kila siku bali hata wafanyabiashara wanalalama
Uongozi wa kata ya Pemba unakiri uwepo wa changamoto hiyo ya barabara lakini unasema tayari serikali ishatoa fedha kwa ajili ya barabara ingawa ni ndogo.
Kwa upande wake mratibu wa wakala wa barabara vijijini (Tarura) Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Godwin Mpinzile anasema wanatambua changamoto wanazokutana nazo wananchi msimu huu wa mvua hasa maeneo ya wilaya za Mvomero na Kilosa.
Licha ya ubovu wa barabara pia kijiji hicho kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mtandao wa simu hatua ambayo inatjwa pia kukwamisha maendeleo ya kijiji hicho cha Pemba
Mwisho