Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amelipongeza bunge kwa kupitisha sheria ya madini inayoelezea mali kama madini kuwa ni mali ya watanzania .
Rais Magufuli amesema hayo wakati akizungumza na wakazi wa Kahama ambapo ameiongeza kampuni ya Barrick ambayo imekubali kuingia ubia na Tanzania kwa kuunda kampuni inayoitwa twiga kwasasa.
Amesema fedha zitakazopatikana kutokana na sekta hiyo ya madini zitaweza kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi kama vile suala la maji, elimu na huduma ya kupata tiba bora.
Kwa upande mwingine Rais Magufuli ametoa onyo kwa wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kutokwenda kukopa pesa benki kwa ajili ya miradi iliyopo katika wilaya zao.
“Na hii ni kwa wakurugenzi wote Tanzania sitaki kuona halimashauri yoyote inakwenda kukkopa hela kwenye benki, na wale ambao wamezikopa wavunje hiyo mikataba.”
Rais Magufuli amekipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa ushindi walioupata katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika novemba 24, mwaka huu na kusisitiza mshikamano kwa wananchi ili kuleta maendeleo kwa taifa.
Mwisho.