Hayo yamebainika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo imeeelezwa, Seth aliandika barua yake iliyopitia kwa Mkuu wa Gereza baada ya msamaha uliotangazwa na Rais Dk John Magufuli.
Wakili wa utetezi, Michael Ngaro anayemtetea Rugemalira amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa mteja wake ameandika barua kwa DPP kuomba kukiri makosa ya uhujumu uchumi yanayomkabili na kwamba mpaka sasa hawajapata majibu. Kufuatia taarifa hiyo Ngaro ameuomba upande wa mashitaka kufanya mchakato ili wapate majibu ya barua hiyo haraka
Akijibu hoja hiyo, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon amedai kuwa, ni kweli wamepokea barua za washtakiwa wote wawili na kwamba zinafanyiwa kazi na watapatiwa majibu.Kutokana na kesi hiyo ambayo ilikuja kwa ajili ya kutajwa, Hakimu Shaidi ameahirishwa hadi Oktoba 24, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa tena
Seth, mwenyekiti mtendaji wa PAP pamoja na James Rugemalira ambaye ni mkurugenzi wa VIP wanakabiliwa na mashtaka 12 wanayodaiwa kuyatenda jijini Dar es Salaam, Afrika Kusini, Kenya na India.Miongoni mwa mashtaka hayo ni kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu , kughushi na kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kusababisha hasara ya Sh 309bilioni.
Washtakiwa hao walifikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama hiyo Juni 19, 2017 na hadi sasa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.