Star Tv

Mwanafunzi mmoja Matutu Mashini (7) aliyekuwa anasoma darasa la kwanza katika shule ya msingi Salama A, iliyoko katika wilaya ya Bunda mkoani Mara, amekufa maji, baada ya kutumbukia katika kisima kirefu wakati akichota maji.

Kwa mujibu wa afisa mtendaji wa kijiji cha Salama A, Mashaka Maulilo, tukio hilo limetokea juzi majira ya saa tano na dakika 20 asubuhi kijijini hapo wakati mtoto huyo pamoja na wenzake watatu wakichota maji katika kisima hicho. Maulilo amesema kuwa wakati mtoto huyo akichota maji chombo chake alichokuwa akitumia kuchota maji kilimtoka mkononi na kwenda katika kina kirefu, ambapo alikifuatilia na kuzidiwa na maji hayo na ndipo akapoteza maisha. Aidha, amesema kuwa wenzake walikwenda kutoa taarifa kwao, ambapo yowe ikapigwa na wananchi wakaenda katika eneo la tukio na kuanza kuutafuta mwili wa marehemu kwa kuzamia katika kisima hicho na ndipo wakafanikiwa kuuopoa na kwenda kuuzika. Afisa mtendaji huyo ametoa wito kwa wazazi na walezi kuacha tabia ya kutuma watoto wadogo kwenda kuchota maji kwenye visima, wakati wakiwa hawana mtu mzima, akisema kuwa kama kungekuwa na mtu mzima mtoto huyo uhenda angeokolewa. 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.