Star Tv

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka, ameitaka Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA,  kutoa elimu kwa wananchi juu ya madhara ya kutumia vyakula, vipodozi  na dawa zilizokwisha muda wake wa matumizi. Ilikuwa ni kikwazo kwa wajasiriamali wadogo mkoani Simiyu kufuata huduma za Mamlaka ya Chakula  Dawa TFDA jijini Mwanza, lakini kwa sasa wamesogezewa huduma karibu mjini Bariadi, pamoja na kupongeza hatua hii, changamoto hazikosekani.

TFDA imezindua ofisi mjini Bariadi kwa ajili kusogeza huduma kwa wananchi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa Mashariki ambayo ni Simiyu, Mara na Shinyanga, ambapo Kaimu Meneja wa Kanda hiyo Nuru Mwasuluma anaelezea namna walivyojipanga kutoa huduma, kubwa kudhibiti ubora na usalama wa vyakula, vipodozi na dawa.

Aidha Mtaka amesisitiza mamlaka hiyo kuangazia zaidi maeneo ya vijijini ambayo kwa muda mrefu yamesahaulika, huku wananchi wakiwa kwenye hatari ya kuuziwa na kutumia bidhaa zilizomaliza muda wake wa matumizi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.