Madiwani halmashauri ya wilaya ya bariadi mkoani Simiyu wameilalamikia serikali kuhusu zao la pamba kukosa soko la uhakika na hivyo kumdidimiza mkulima.
malalamiko hayo wameyatoa katika mkutano wa baraza la madiwani wa kujadili na kupitisha taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo ngazi za kata.
Wanaona kukosekana kwa soko la uhakika la zao la pamba kunamsababishia hasara mkulima aliyotumia wakati wa kilimo jambo ambalo linakuwa kinyume na kauli mbiu ya ‘Pamba ni Dhahabu Nyeupe.
Huku bi Penina mponeja diwani viti maalumu kutoka kata ya Dutwa ameitaka serikali kuchukua hatua kwa wafanyabiashara wadogo maarufu kwa jina la machinga kulangua pamba ya wakulima kwa bei tofauti na ile elekezi.