Star Tv

Kamati ya ulinzi na usalama wilayani Uvinza imetoa onyo kwa wajumbe wa kamati ya usimamizi wa mpango wa TASAF Ngazi ya vijiji CMC kuchukua pesa zinazotolewa za kuwalenga
wanufaika wa TASAF na kuzitumia kinyemela na kuahidi kuchuku hatua kali za kinidhamu na Kisheria kwa mtu yeyote atakaye bainika kufanya hivyo.

Kamati hiyo ya ulinzi na usalama wilaya ya Uvinza imetoa Onyo hilo huku kukiwa na kumbukumbu ya hapo mwaka jana kukamatwa na  kutiwa hatiani kwa Wajumbe wa kamati ya usimamaizi ya TASAF ngazi ya kijijji katika kata za Ilagala na Muleala wilayani humo baada ya kubainika kutumia nafasi zao kusainia na kuchukulia pesa za Wanufika. Onyo hilo limetolewa kupitia mikutano ya hadhara Kwa wanufakia wa TASAF katika vijiji vya Nguruka Bweru na Nyagambo wilayani Uvinza wakati ziara ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya Ilipopita kukagua utekelezaji wa TASAF. Huku mratibu wa TASAF halmashauri ya wilaya ya Uvinza Dismas Clement amelazimika kutoa ufafanuzi juu ya malalamiko ya baadhi ya wanufaikia kuwepo Upendeleo katika utoaji wa Ruzuku.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.