Mahakama kuu kanda ya Musoma mkoani Mara imeanza kusikiliza kesi 15 za mauaji ya kukusudia na yasiyo ya kukusudia toka kwa watuhumiwa mbali mbali waliopo ndani ya magereza kwa muda wa wiki moja zikiwemo kesi nane toka mahakama kuu kanda ya Mwanza zilizokuwa zimeelekezwa huko ili ziweze kusikilizwa na kutolewa maamuzi.
Jaji mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Musoma mkoani Mara,mheshimiwa John Kayoza amesema kuwa wanataraji kusikiliza kesi 15 za mauaji ambazo zilifunguliwa awali lakini na mpya ambazo zimefunguliwa tokea mwezi wa pili mwaka huu. 'Ujio wa mahakama kuu kanda ya Musoma mkoani Mara unataraji kuwasaidia wananchi waliokuwa wakishindwa kwenda jijini Mwanza kuudhulia vikao vya kesi kutokana na kutokuwa na fedha za kuwawesha kufanya hivyo na sasa serikali imewasogezea huduma hiyo muhimu jirani yao, amesema Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dk, Vicenty Aney. Mahakama kuu kanda ya Musoma Mara imeanza kikao chake cha kwanza cha kusikilizxa kesi kumi na tano za mauaji huku ikitaraji baada ya wiki mbili kuketi na majaji watatu kusikiliza kesi mbali mbali zilizotoka kanda ya mwanza na kuzitolea maamuzi.