Star Tv

Mahakama kuu kanda ya Musoma mkoani Mara imeanza kusikiliza kesi 15 za mauaji ya kukusudia na yasiyo ya kukusudia toka kwa watuhumiwa mbali mbali waliopo ndani ya magereza kwa muda wa wiki moja zikiwemo kesi nane toka mahakama kuu kanda ya Mwanza zilizokuwa zimeelekezwa huko ili ziweze kusikilizwa na kutolewa maamuzi.

Jaji mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Musoma mkoani Mara,mheshimiwa John Kayoza amesema kuwa wanataraji kusikiliza kesi 15 za mauaji ambazo zilifunguliwa awali lakini na mpya ambazo zimefunguliwa tokea mwezi wa pili mwaka huu. 'Ujio wa mahakama kuu kanda ya Musoma mkoani Mara unataraji kuwasaidia wananchi waliokuwa wakishindwa kwenda jijini Mwanza kuudhulia vikao vya kesi kutokana na kutokuwa na fedha za kuwawesha kufanya hivyo na sasa serikali imewasogezea huduma hiyo muhimu jirani yao, amesema Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dk, Vicenty Aney. Mahakama kuu kanda ya Musoma Mara imeanza kikao chake cha kwanza cha kusikilizxa kesi kumi na tano za mauaji huku ikitaraji baada ya wiki mbili kuketi na majaji watatu kusikiliza kesi mbali mbali zilizotoka kanda ya mwanza na kuzitolea maamuzi.

  

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.