Star Tv
Wananchi zaidi ya 40 wakiwemo madiwani kuandamana  zaidi ya kilometa 120 hadi ofisi ya mkuu wa mkoa wa Geita june 3 kupinga njama za kutaka kupokonywa ardhi inayozalisha madini ya dhahabu katika machimbo ya Nyakafulu wilayani Mbogwe Mkoani Geita, ambapo tukio hilo limechukua sura mpya baada ya mkuu wa mkoa kutangaza  kuunda kamati kuchunguza madai hayo.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amesema ameamua kuunda kamati itakayovihusisha pia vyombo vya usalama kutokana na malalamiko ya walioandamana kuwatuhumu baadhi ya viongozi wa serikali kuu , halmashauri ya wilaya ya Mbogwe , chama cha mapinduzi na matajiri kuwa ndio walioko nyuma ya mgogoro huo ili kuwapokonya ardhi ambayo tayari ina uzalishaji wa madini ya dhahabu katika kijiji cha Nyakafulu. Mhandisi Robert Gabriel amesema kamati hiyo itachunguza na kuwahoji wote wanaotajwa kuwa nyuma ya mgogoro huo huku shauri lililotolewa uamuzi na Baraza la Ardhi na Nyumba la kata uliochangia kuibua maandamano hayo ameelekeza mdaiwa kukata rufaa katika Baraza la ardhi na nyumba la wilaya kwa hatua zaidi za kisheria.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.