Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kesho tarehe 07 Juni, 2019 atakutana na wafanyabiashara kutoka Wilaya zote hapa nchini na wajumbe wa Baraza la Biashara la Taifa (TNBC). Wafanyabiashara watano kutoka kila Wilaya hapa nchini watawawakilisha wafanyabiashara wenzao. Mkutano huo utaanza saa 3:30 asubuhi na kurushwa moja kwa moja kupitia vyombo vya habari vya Redio, Televisheni na Youtube Channel ya Ikulumawasiliano.
CHANZO: Ikulu Mawasiliano.