Star Tv

Ushauri umetolewa kwa wanaume walioko katika wilaya ya Bunda mkoani Mara, kujenga tabia ya kuwasaidia wake zao, ambao ni wajawazito kwa kuwapeleka kliniki na kusikiliza ushauri wa wauguzi, badala ya kuwaacha wenyewe tu kwa kudhani kuwa jukumu hilo ni la mwanamke mwenyewe.

Ushauri huo umetolewa na baadhi ya wanaume waliojitokeza kwenye maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani, yaliyofanyika katika viwanja vya kituo cha afya cha Bunda mjini kilichoko katika kata ya Kabarimu katika  halmashauri ya mji wa Bunda. Aidha, baadhi ya wanawake wameizungumzia siku hiyo ya wauguzi duniani, huku wakiwaomba wauguzi kutekeleza wajibu wao ipasavyo, hasa wakati wakimuhudumia mama mjamzito. Baadhi ya wauguzi wamesema kuwa wamekuwa wakikumbana na changamoto mbalimbali pindi wanapopokea wagonjwa wakiwemo wajawazito, ikiwa ni pamoja na kutukanwa na baadhi ya watu. Katika maadhimisho hayo mkuu wa wilaya ya Bunda Lydia Bupilipili, amewataka wauuguzi wote wilayani hapo kutekeleza wajibu wao ipasavyo ikiwa ni pamoja na kujiamini.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.